Ofisa Masoko wa Jiji hilo, James Yuna amesema maeneo kama barabara za magari na watembea kwa miguu, darajani na mitaroni ni hatari wafanyabiashara na wateja, hivyo wafanye biashara kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya biashara hizo badala ya kuvamia maeneo yasiyo rasmi kwao.
Aliwataka viongozi wao kushirikiana na jiji kutoa elimu, ili kuondoa tatizo la kufanya biashara bila mpangilio wowote.
Ofisa huyo pia aliwataka wafanyabiashara kufanya biashara kwenye masoko yaliyoko karibu kwenye kata zote kwa kuwa nafasi bado zinapatikana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |