Wakulima wanahofia kwamba wadudu hao wataharibu kabisa mimea ambayo walipanda majuzi. Maeneo yaliyoathiriwa zaidi ni Kimbimbi, Mathangauta, Thiba, Kiorugari, Murubara na Nguka ambako mchele hukuzwa kwa wingi.
Mradi wa Mwea ni wa ekari 30,350 ambapo ekari 22,000 zinakuzwa mchele huku zilizosalia zikitumiwa kwa makao na kilimo cha mimea mingine ya chakula.
Kulingana na wakulima, konokono hao wanakula mimea yao na kuwasababishia hasara kubwa. Mwea ndilo eneo linalokuza mchele kwa wingi nchini Kenya na wakulima wanahofia kuwa huenda wadudu hao wakaharibu mimea yao yote ikiwa hatua za kuwaangamiza hazitachukuliwa.
Wakulima hao wanaomba serikali ya Kaunti ya Kirinyaga kuwasaidia kuangamiza wadudu hao kwa sababu kilimo kimegatuliwa.
Walisema wanategemea mchele kulisha na kusomesha watoto wao na hivyo basi serikali inafaa kuchukua hatua za haraka kuwatafutia suluhu ya tatizo la konokono hao. Mradi wa Mwea hutoa asilimia 80 ya mchele wote unaokuzwa nchini..
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |