Mawaziri wa biashara na uwekezaji wa Kundi la Nchi 20 G20 wameapa kuhakikisha ugavi wa bidhaa muhimu, hasa vifaa vya tiba na dawa, wakati dunia nzima inakabiliwa na msukosuko wa virusi vya Corona.
Taarifa iliyotolewa na mawaziri hao kwenye tovuti ya Sekritarieti Kuu ya G20, imefuatilia changamoto zinazowakabili wafanyakazi na biashara, haswa wale walioko hatarini zaidi.
Taarifa pia imesisitiza juhudi za mwitikio wa pamoja unaounga mkono makampuni madogo na yenye ukubwa wa kati, na kutambua umuhimu wa kuimarisha uwekezaji wa kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |