Rais Xi Jinping wa China amesisitiza ulinzi wa mazingira ya ikolojia, na kusema juhudi zote za ulinzi wa ikolojia zitazawadiwa.
Rais Xi, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China, amesema hayo alipotembelea kijiji cha Yucun, kilichoko kaunti ya Anji, mkoa wa Zhejiang, mashariki mwa China hapo jana.
Amesema kulinda vizuri milima na mito kutawasaidia watu kuwa na fursa ya kipekee ya maendeleo ya uchumi, na kuongeza kuwa mazingira ya ikolojia yenyewe ni uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |