Uongozi wa Klabu ya Azam umesema uko tayari kumuuza kiungo wao, Salum Abubakar 'Sure Boy' kwa Yanga au klabu yoyote inayomuhitaji kama wataenda mezani na kuafikiana kuhusu dau la mchezaji huyo. Sure Boy amecheza kwa mafanikio makubwa katika kikosi cha Azam FC kwa kipindi cha zaidi ya miaka 10 sasa huku kukiwa na taarifa ya Yanga kuhitaji huduma yake. Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema wako tayari kumuuza mchezaji huyo, hivyo wanamkaribisha yeyote anayemtaka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |