• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • UNCTAD yatia wito wa kuendelea kwa uchukuzi wa baharini

    (GMT+08:00) 2020-04-01 18:55:28
    Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (Unctad) limemetoa wito wa kuendelea kwa biashara ya uchukuzi wa majini hata wakati huu dunia ikikabili virusi vya corona.

    Katika taarifa ya Katibu Mkuu wa shirika hilo Mukhisa Kituyi alisema wakati ulimwengu unapambana na janga hilo, tasnia ya uchukuzi wa baharini duniani inachukua jukumu muhimu kutoa mchango wake.

    Kituyi amesema karibu asilimia 80 ya biashara ya kimataifa hutegemea uchukuzi wa baharini kusafirisha chakula, nishati na malighafi za ulimwengu.

    Alisema kuwa katika wakati huu wa mzozo duniani, ni muhimu zaidi kuweka minyororo ya usambazaji wazi na kuruhusu biashara ya baharini na usafirishaji baiana ya nchi kuendelea.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako