Serikali ya Zambia imetangaza kuwa maporomoko ya maji ya Victoria ambayo ni urithi wa dunia, yamefungwa mara moja kwa muda usiojulikana. Katika barua iliyosainiwa na kutolewa na mkurugenzi wa kanda wa kamati ya uhifadhi na urithi wa kitaifa ya nchi hiyo Bw. Oliver Kandyata kwa Shirikisho la utalii la Livingstone, amesema kufungwa kwa maporomoko hayo kunatokana na mlipuko wa virusi vya Corona.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |