• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Malima amtaka Gadiel aondoke Simba

    (GMT+08:00) 2020-04-02 16:42:37

    Mchezaji wa zamani wa Yanga na timu ya taifa Tanzania Taifa Stars, Bakari Malima amemshauri beki wa Simba Gadiel Michael kuangalia uwezekano wa kuhamia timu nyingine katika msimu ujao. Malima alesema kuwa, Gadiel ana kipaji na ili akinoe, anatakiwa kuondoka Simba alikoshindwa kutamba mbele ya Mohammed Hussein ambaye anaaminiwa kwenye kikosi cha kwanza. Amesema Gadiel ni miongoni mwa wachezaji vijana ambao wanapaswa kuitumikia timu ya taifa akiwa kwenye ushindani wa kiwango cha juu, na kusisitiza kwamba, kukaa kwake benchi hakutoi picha nzuri kwake.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako