Serikali ya China leo imetangaza kuwa, ili kutoa rambirambi kwa mashujaa na ndugu waliofariki katika mapambano dhidi ya virusi vya Corona, China itafanya shughuli ya maombolezo ya kitaifa kesho tarehe 4, Aprili.
Katika muda huo nchini kote na balozi za China katika nchi za nje, bendera zitapepea nusu mlingoti, na kusimamisha shughuli zote za burudani kote nchini. Kuanzia Saa 4 asubuhi ya kesho, wachina wote watakaa kimya kwa muda wa dakika 3, na ving'ora, honi za magari, trenii na meli zitapigwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |