Kwa mujibu wa takwimu mpya za Kituo cha Sayansi na Uhandisi cha Chuo Kikuu cha Johns Hopkins, hadi kufikia Jumamosi jioni idadi ya wagonjwa wa Corona duniani imeongezeka na kufikia milioni 1.2, na watu 64,703 wamekufa na ugonjwa huo.
Marekani imeripoti idadi kubwa zaidi duniani, ambayo ni 311,301, ikifuatiwa na Uhispania yenye wagonjwa 126,168 na vifo 11,947.
Italia imeripoti wagonjwa 124,632 ikiwa na idadi kubwa kabisa ya vifo duniani 15,362.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |