Timu ya madaktari ya China imewasili Nur-Sultan, mji mkuu wa Kazakhstan, ili kuisaidia nchi hiyo kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona. Timu hiyo inayoundwa na watu kumi imeenda na msaada wa matibabu, ikiwemo maski 4800 aina ya N95, maski 49600 za ngazi ya upasuaji, nguo 2,000 za kujikinga, mashine mbili za kupumulia na dawa nyingine nyingi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |