• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • CORONA: Barcelona yapanga kuuza kwa muda haki ya jina la uwanja Nou Camp

    (GMT+08:00) 2020-04-22 08:09:44

    Barcelona ina mpango wa kuuza haki ya jina la uwanja Nou Camp kwa muda wa mwaka mmoja ili kupata fedha zitakazoweza kuwasaidia katika vita vya kiuchumi dhidi ya janga la virusi vya corona. Kuuzwa kwa jina hilo Nou Camp, kutaweza kushuhudiwa moja kati ya viwanja vyenye historia kubwa katika mchezo wa soka duniani vikianza kupoteza tamaduni zake. Bodi ya utendaji ndani ya Barcelona, Jumanne imesema klabu itakusanya fedha zote zitakazotokana na mauzo ya haki ya jina Nou Camp ili kusaidia vita dhidi ya virusi vya corona. Nou Camp ni moja ya uwanja mkubwa kabisa barani Ulaya, wenye viti zaidi ya 99,000 na haukuwahi kuwa na mdhamini tangu kufunguliwa kwake mwaka 1957. Klabu itasubiri kuuza haki ya jina la uwanja huo kwa mara ya kwanza ifikapo msimu wa mwaka 2023-24. Katika muda huo Barcelona inaamini itaweza kuingiza kitita cha fedha paundi milioni 264. Baadhi ya mashabiki wa klabu hiyo ya Barcelona wanaamini kuwa huo ndiyo utakuwa mwanzo wa kupotea kwa tamaduni za uwanja wao. Makamu wa Rais wa Barcelona amesema wanataka kuwatumia ujumbe watu wote. Kwa mara ya kwanza mtu atakuwa na nafasi ya kuweka jina lake Nou Camp.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako