Rais wa Chama cha Golf Wanawake nchini Tanzania Sophia Reiffenstein amesema, pindi serikali itakaporuhusu michezo kurejea nchini humo, mikakati Yo ni kuhakikisha wanafanikiwa kufufua klabu zote zilizokufa katika mchezo huo. Serikali ya Tanzania ilipiga marufuku shughuli zote zinazosababisha mikusanyiko ya watu nchini humo tangu Machi 17 mwaka huu, ikiwemo michezo, kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona. Sophia amesema, hadi sasa wamefanikiwa kufufua klabu moja tu ya Lugalo ya jijini Dar es Salaam ambayo walifanya uchaguzi wao kabla ya janga la Corona na kupata viongozi wapya. Pia amesema, moja ya mkakati wao ni kuhakikisha timu ya Golf ya Wanawake inakwenda Libya kushiriki michuano ya Chalenji Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |