Shaquille O'Neal, mchezaji wa zamani wa mpira wa kikapu na mshindi mara nne wa Ligi hiyo nchini Marekani NBA amesema itakuwa busara kama msimu wa 2019/20 uliosimamishwa kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona utafutwa. Amesema wachezaji wa Ligi hiyo wanapaswa kuanza maandalizi kwa ajili ya msimu wa 2020/21 na kuachana na mashindano yaliyoahirishwa mwezi Machi kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona. Amependekeza ligi hiyo ifutwe, wachezaji na wakufunze wakae nyumbani, walinde afya zao, na kurejea mwaka ujao katika msimu mwingine, na kutaka kwanza afya ya mashabiki na wachezaji izingatiwe.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |