Jana Baraza la sanaa la Taifa BMT lilitangaza rasmi kuanza kuchukua maoni kuhusiana na mapendekezo yaliyotolewa na serikali kuhusiana vilabu vya soka Tanzania kupunguza idadi ya wachezaji wa kigeni wanaosajiliwa. Kwa sasa timu moja Tanzania inaruhusiwa kusajili wachezaji kumi tu wakigeni lakini serikali kupitia waziri mwenye dhamana ya michezo Dr Harison Mwakyembe wamependekeza idadi ipungue na sasa wanapokea maoni ili watangaze rasmi idadi itakuwa ngapi. Lakini wadau wa soka wamekuwa na maoni tofauti. Golikipa Juma Kaseja anaonekana kutokubaliana na uamuzi wa kupunguza idadi ya wachezaji wa kigeni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |