Uchunguzi alioufanya Shigella umetokana na zaidi ya magari 10 ya abiria na magari 40 ya mizigo yaliyokuwa yakisafiri kwenda Mombasa nchini Kenya, kuzuiwa katika mpaka wa Lungalunga upande wa Kenya hadi abiria na madereva wapimwe virusi vya corona na kusubiri majibu kwa muda wa siku tatu.
Uamuzi huo umetokea usiku wa Jumatatu hadi Jumanne ambako hatua imesababisha baadhi ya Watanzania hao kugomea vipimo vya corona vya Kenya hadi kuwepo madaktari Watanzania.
Kutokana na hali hiyo, baadhi ya abiria waliokuwa wakienda Mombasa waligoma kupima na kuamua kurudi Tanga.
Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Shigella alifanya ziara mpakani hapo kujionea hali halisi.
Aliwasisitiza maofisa wa Horohoro kutoa ushirikiano na wenzao wa Kenya bila kuathiri taratibu za mipaka za Tanzania na Kenya ili kuondoa changamoto hiyo pamoja na kuweka tahadhari za kujikinga.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |