Katibu Mkuu wa shirikisho la soka Tanzania TFF Wilfred Kidao ameongea na vyombo vya habari jana kuhusiana na mambo mbalimbali ikiwemo kutolea ufafanuzi kuhusiana na tuhuma dhidi ya viongozi wa TFF zilizotolewa hivi karibuni kuwa wanatumia pesa za FIFA kinyume na taratibu. Kidao amesema Shirikisho la soka Duniani FIFA, kila mwaka wanaipa Tanzania Bil 2.3 ambazo hutoka kwa awamu mbili yaani Januari na Julai na huwa unafanyika ukaguzi wa matumizi ya awamu iliyopita kabla ya kupewa tena.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |