Winga wa zamani wa Barcelona, Trevor Sinclair amesema kuwa huenda kocha Guardiola akarejea ndani ya klabu hiyo. Guardiola yupo ndani ya Manchester City na aliinoa Barcelona 2008 mpaka 2012 ambapo aliweza kutwaa mataji kadhaa ikiwa ni pamoja na lile la Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mkataba wake na City unatarajiwa kumalizika mwaka 2021 na inaelezwa kuwa anataka kusepa. Winga huyo amesema ishu ya Guardiola kurejea Barcelona ni suala la muda tu kwa sasa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |