Pilipili ni kati ya bidhaa za Rwanda zinazosafirishwa kwenda China chini ya Jukwaa la elektroniki la Biashara Ulimwenguni (eWTP).
Rwanda na Alibaba mnamo 2018 walitia saini makubaliano ambayo yalifungua milango kwa biashara ndogo ndogo barani Afrika kushiriki katika biashara ya kieletroniki kwa kuuza bidhaa zao kwenye soko la China kupitia jukwaa la eWTP.
Katika mwaka wa fedha wa 2018-2019, Rwanda ilipata dola milioni moja kutoka kwa mauzo ya nje ya pilipili, kulingana na takwimu kutoka kwa Bodi ya Kitaifa ya Maendeleo ya Uuzaji wa Kilimo (NAEB).
Mwaka huo huo Rwanda ilisafirisha nje kilo 721,000 za pilipili, ambayo inaonyesha uwezekano wa kupanda kwa mazao katikati ya juhudi za nchi hiyo za kuongeza mauzo yake.
Mwaka jana, mjasiriamali wa kilimo nchini Rwanda, alianza kusambaza tani 100,000 za pilipili zilizokaushwa zenye thamani ya dola milioni 100 (karibu bilioni bilioni Rwf) kila mwaka kwenda China, hatua inayotarajiwa kuongeza usafirishaji wa kilimo nchini Rwanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |