Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania, Wilfred Kidau amehojiwa jana na Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Tanzania (Takukuru). Kidau alionekana akiingia ofisini majira ya saa tatu dk 42 na alitoka saa tano dk 14. Inaelezwa kuwa sababu ya kuitwa Takukuru ni kuhojiwa kutokana na matumizi ya Tsh. Bilioni 1 zilizotolewa kwa ajili ya AFCON 2019 ya vijana. TFF ilidai kuwa fedha hizo zilizotolewa na Rais Magufuli hazikuingia katika akaunti zao. Inadaiwa kuwa Kidao ameitwa kama sehemu ya mashahidi wanaotakiwa kutoa maelezo yao kuhusiana na fedha hizo ili kujua zilitumikaje licha ya kuwa hazikupita katika account ya TFF.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |