• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • CHESS: Mcheza chess wa Tanzania afurahia nafasi katika mashindano ya Afrika

    (GMT+08:00) 2020-05-20 17:24:56

    Mchezaji wa Chess kutoka nchini Tanzania Albert Njau ameeleza uzoefu wake katika mashindano ya bure ya Chess kupitia mtandao wa internet kuwa ni kumbukumbu nzuri kwake. Njau, ambaye ni Mtanzania pekee aliyeshiriki katika mashindano hayo yaliyovutia wachezaji wazoefu zaidi ya 1377, alipata alama 28 kutoka michezo 15 na kumaliza wa 125. Alishinda michezo kumi na kupoteza mitano. Shirikisho la Mchezo wa Chess barani Afrika (ACF) liliandaa mashindano hayo kupitia mtandao wa internet kama majaribio ya mchezo huo wakati dunia ikikabiliwa na janga la mlipuko wa virusi vya Corona. Katika shindano hilo, mchezaji kutoka Malawi Fide Master aliibuka mshindi kwa kupata pointi 64.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako