• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya yazindua kanuni mpya kuboresha uzalishaji wa chai

    (GMT+08:00) 2020-05-22 08:55:25

    Wizara ya kilimo ya Kenya jana Alhamisi ilizindua kanuni mpya kusaidia kuongeza tija kwenye sekta ya chai, kuinua ufanisi katika mnyororo wa thamani na kuweka uwazi kwenye sekta hiyo.

    Waziri wa Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Ushirika nchini Kenya Bw. Peter Munya amesema kanuni mpya zinahitaji viwanda vyote vya chai kujiandikisha kwa serikali na waandaaji wa mnada ili kushiriki kwenye mnada wa chai moja kwa moja.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako