Rais Xi Jinping wa China amesema nchi yake haijali hasara kubwa namna gani inayopata katika kulinda maisha, usalama na afya ya watu wake.
Rais Xi ameyasema hayo leo aliposhiriki kwenye majadiliano ya wajumbe wa Bunge la 13 la Umma la China NPC kutoka Mkoa Unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani. Amesema msingi wa Chama cha Kikomunisti cha China CPC ni watu, hivyo wazo la kutoa kipaumbele kwa wananchi halitabadilika daima bila kujali kuna changamoto na shinikizo gani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |