Walisema hayo baada ya Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, kuwasha umeme katika kijiji hicho na kukagua maendeleo ya usambazaji umeme.
Walisema, kwa miaka mingi wamekuwa wakipewa ahadi zisizotekelezeka na wakati mwingine wakikatishwa tamaa ya kupata umeme kwa kuwa kijiji hicho kiko umbali mrefu kutoka ilipo miundombinu ya umeme na jiografia isiyo rafiki kufika maeneo hayo.
Dk. Kalemani kwa upande wake alisema baada ya kusikia malalamiko na kuona uhitaji mkubwa wa umeme kwa kijiji hicho ambacho hakijafikiwa na mradi wa kusambaza umeme (REA) kwa kipindi hiki, aliliagiza Shirika la Umeme nchini humo (Tanesco) kupeleka umeme kwa gharama zao katika kijiji hicho.
Alisema kijiji cha Loya kina wakulima wengi wa mpunga, karanga na wafanyabiashara ambao wanahitaji huduma ya umeme katika kuendesha shughuli zao za kiuchumi.
Tanesco ilitenga zaidi ya Sh. bilioni tatu ili kuhakikisha umeme unafika katika kijiji hicho, ambacho kiko umbali mrefu kutoka ilipopita miundombinu ya umeme.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |