Kwa mujibu wa Ofisi ya mkoa wa Mbeya, mkutano mkuu wa Kijiji ndio wenye mamlaka ya kugawa ardhi ya kijiji.
Ofisi hiyo imesema kazi ya viongozi wa vijiji hasa ofisa mtendaji na mwenyekiti ni kupokea maombi ya wanaotaka kupewa ardhi na kuitisha mikutano ya vijiji ili wananchi wajadili na kuridhia ama kutoridhia kugawa ardhi yao kulingana na uhitaji.
Kwa mujibu wa sheria ya ardhi, kijiji kinaruhusiwa kugawa ardhi isiyozidi hekta 50 kwa mtu mwingine na kwamba ikizidi ukubwa huo zipo mamlaka zingine ambazo zinahusika na hivyo mhitaji wa ardhi hiyo atatakiwa kuziona.
Kuhusu mpango wa matumizi bora ya ardhi, kila kijiji kinatakiwa kuwa na matumizi bora ya ardhi kwa maelezo kuwa utaratibu huo unasaidia kuondoa migogoro ya ardhi kwa kuepusha mwingiliano wa shughuli za kibinadamu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |