Rais Xi Jinping wa China jana alihudhuria mjadala wa wajumbe wa sekta ya uchumi wanaoshiriki kwenye mkutano wa mwaka wa baraza la mashauriano ya kisiasa.
Rais Xi amesema Mkutano wa tatu wa wajumbe wote wa kamati kuu ya 18 ya Chama cha Kikomunisti cha China uliamua kulifanya soko lifanye kazi ya msingi kwenye mgawanyo wa rasilimali, lakini pia serikali inapaswa kufanya vizuri kazi yake. Uzoefu wa mageuzi umeonyesha kuwa ni lazima kazi ya soko na ya serikali ziunganishwe vizuri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |