Waziri wa Hazina ya Ukur Yatani amesema kuwa serikali ilikuwa makini na suluhisho la muda mrefu aidha amesema kwamba shida za kifedha za shirika hilo ni zaidi ya shida zinazohusiana na Corona.
Shirika la Kitaifa anahitaji pesa kwa ajili ya matengenezo ya ndege, malipo ya mishahara ya wafanyikazi na malipo ya bili za matumizi.
Kufungiwa kwa ndege zote za abiria kuanzia Machi 22 na kizuizi cha kutoka na kuingia katika maeneo manne yakiwemo Nairobi, Mombasa, Kwale na Kilifi ili kumaliza kuenea kwa virusi imeumiza biashara ya shirika la ndege la Kenya Airways vibaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |