Kituo cha Kinga na Udhibiti wa Magonjwa cha Afrika (Africa CDC) kimesema, hadi kufikia jana idadi ya watu walioambukizwa virusi vya Corona barani Afrika imefikia 141,535, huku idadi ya vifo ikiongezeka hadi kufikia 4,069, na wagonjwa takriban 59,212 wamepona.
Kituo cha Africa CDC kimeongeza kuwa hadi sasa virusi vya Corona vimesambaa kwenye nchi 54 za Afrika, na eneo la kaskazini mwa Afrika ndio lililoathiriwa zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |