Rais Vladimir Putin wa Russia na mwenzake wa Marekani Bw. Donald Trump wamefanya mazungumzo kwa njia ya simu jana Jumatatu, ambapo rais Trump alimwarifu rais Putin kuhusu mpango wake wa kuwaalika viongozi wa Russia, Australia, India na Korea Kusini kuhudhuria mkutano wa kilele wa G7.
Russia imetoa jibu kuwa nia ya kuhudhuria mkutano huo au la, inategemea nafasi yake kwenye mkutano huo, kwa hiyo itasubiri maelezo zaidi kutoka kwa upande wa Marekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |