Matokeo ya uchunguzi wa mwili uliofanywa na Ofisi ya uchunguzi wa kimatibabu ya polisi ya jimbo la Minnesota na wanasheria walioajiriwa na jamaa wa Bw. Floyd yote yamethibitisha kuwa Bw. Floyd alifariki kwa mauaji.
Gavana wa Jimbo la Minnesota Bw. Tim Walz amesema, jimbo hilo limeanzisha uchunguzi wa haki za kiraia kwa Idara ya Polisi ya jimbo hilo MPD, ambapo maofisa wanne wa polisi walihusishwa na mauaji hayo ya kikatili.
Bw. Walz amesema Idara ya Haki za Binadamu ya Minnesota imewasilisha mashtaka ya haki za kiraia dhidi ya MPD na itachunguza "sera, taratibu na vitendo vyake katika miaka 10 iliyopita ili kuthibitisha kuwa kama walifanya vitendo vya ubaguzi wa kimfumo. "
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |