• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Eastleigh yaamka tena kibiashara

    (GMT+08:00) 2020-06-09 16:35:23
    Mtaa wa Eastleigh, Nairobi, Jumapili ulirejelea hali yake ya kawaida huku wenye biashara wakifungua saa chache baada ya Rais Uhuru Kenyatta kusitisha amri ya kutoingia na kutotoka eneo hilo.

    Kulingana na data kutoka idara za serikali biashara ya thamani ya takriban Sh200 milioni huendeshwa katika eneo hilo kila siku.

    Baada ya tamko la rais, malori yameanza kuleta bidhaa za kuuza, huku wahudumu wa matatu na waendeshaji wa bodaboda wakirejelea hudumu za kuwasafirisha watu.

    Eastleigh na Old Town Mombasa ni maeneo yaliyofungwa mwezi mmoja uliopita baada ya kuandikisha idadi kubwa zaidi ya maambukizi ya virusi vya corona.

    Hatua hiyo iliathiri uchumi wa Eastleigh; eneo ambalo ni la pili kwa ukubwa kibiashara Nairobi, baada ya Westlands.

    Takwimu kutoka Shirika la Kitaifa la Takwimu (KNBS) zinaonyesha kuwa Eastleigh huchangia asilimia 25 ya jumla ya mapato ya Kaunti ya Nairobi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako