Serikali ya Nigeria imesema watu milioni 40 wa nchi hiyo wanakadiriwa kupoteza ajira zao kabla ya mwisho wa mwaka huu, kutokana na hatua za zuio na kudumisha umbali wa kijamii zilizochukuliwa kuzuia kuenea kwa COVID-19.
Makamu wa rais Yemi Osinbajo akinukuu takwimu za Shirika la Takwimu la Taifa NBS, amesema wanigeria milioni 39.4, ambao ni asilimia 33.6 ya jumla ya watu wa nchi hiyo, wanaweza kuathiriwa na janga hilo, na wengine wengi zaidi wanakadiriwa kuangukia katika ufakara kabla ya janga hilo kumalizika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |