Kenya imeipongeza kampuni ya teknolojia ya China Huawei kwa kusaidia kuongeza maarifa yake kuhusu teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA.
Mamlaka ya TEHAMA nchini Kenya imesema kupitia taarifa iliyotoa jana mjini Nairobi kuwa Huawei imekuwa mwezi muhimu katika mpango wa Vipaji vya Kidijitali (DigiTalents), unaolenga kutafuta watu wenye vipaji vya TEHAMA nchini humo. Mamlaka hiyo imeanza kusajili kundi la tano la watu wenye vipaji kwa mpango huo, na pia imetoa wito kwa Huawei kutoa mafunzo ya kisasa kwa wanafunzi hao.
Huawei imejenga uhusiano wa kiwenzi wa mafunzo na vyuo vikuu na taasisi zaidi ya 30 na hadi sasa wanafunzi zaidi ya 1,200 kutoka Mpango huo wamepewa mafunzo hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |