• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Soko kubwa la jumla la Beijing lafungwa kwa muda baada ya wafanyakazi na watu wa karibu kukutwa na virusi vya Corona

    (GMT+08:00) 2020-06-13 18:53:04

    Soko kubwa la biashara ya jumla ya matunda, mbogambonga na nyama la Beijing Xinfadi, limefungwa kwa muda na kupuliziwa dawa baada ya watu wanaofanya kazi kwenye soko hilo na mazingira yake kugunduliwa kuwa na virusi vya Corona.

    Msemaji wa kamati ya afya manispaa ya Beijing, amesema watu wote waliokaribia soko hilo tangu Mei 30 watafanyiwa upimaji. Amesema kwa sasa mji wa Beijing una vituo 98 vikiwa na uwezo wa kupima watu elfu 90 kwa siku.

    Ijumaa Beijing ilitangaza watu sita wamethibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona. Watu hao na mmoja aliyetangazwa kuambukizwa alhamisi wote wana uhusiano na soko la Xinfadi au watu wa karibu wana uhusiano na soko hilo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako