Wizara ya afya ya Uganda jana jumapili imeripoti maambukizi 11 mapya ya COVID-19, na kuifanya idadi ya jumla ya maambukizi nchini humo kufikia 696. Kwa mujibu wa wizara hiyo, madereva wengine sita wa malori wa Uganda walioingia nchini kupitia vituo vya mpakani vya Elegu na Malaba, walithibitika kuwa na virusi vya Corona.
Aidha, madereva 33 wa malori kutoka nchi za nje waliopimwa na kukutwa na virusi vya Corona kwenye vituo vya mpakani vya Uganda, walikabidhiwa kwa nchi walizotoka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |