Rais Macron wa Ufaransa ametoa hotuba kwa njia ya televisheni, akitangaza hatua kadhaa za kuendelea kulegeza zuio la nchi hiyo la kupambana na virusi la Corona.
Hii ni hotuba ya nne ya televisheni kwa taifa aliyotoa Rais Macron tangu mlipuko wa COVID-19 utokee nchini Ufaransa, akisema kuanzia tarehe 15 mwezi huu, kazi ya kuzuia na kudhibiti janga la COVID-19 nchini Ufaransa itafungua ukurasa mpya.
Rais Macron amesema kuwa Ufaransa haitaongeza viwango vya kodi, na hatua zote zinatakiwa kuchukuliwa ili kuepuka kampuni kupunguza wafanyakazi, kuongeza nafasi mpya za ajira na kujenga uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |