Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo (UNCTAD) limetoa Ripoti ya Uwekezaji Duniani kwa Mwaka 2020. Ripoti hiyo inakadiria kuwa uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nchi za nje duniani kwa mwaka 2020 utapungua kwa asilimia 40 kuliko mwaka jana, na janga la COVID-19 litaufanya uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nchi za nje duniani kutofikia dola za kimarekani trilioni 1 kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2005. Ripoti hiyo imekadiria kuwa uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nchi za nje kwenye nchi zinazoendelea umeathiriwa vibaya zaidi, na hautafufuka kabla ya mwaka 2022.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |