• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Juhudi za kutafuta chanjo na tiba ya virusi vya corona zashika kasi

    (GMT+08:00) 2020-06-17 10:58:55
    Watafiti wanaendelea na juhudi za kutafuta chanjo na vile vile tiba ya virusi vya corona. Mataifa mengi ikiwemo China yametoa mchango mkubwa wa kifedha ili kufadhili harakati hii na tayari kuna chanjo amabazo ziko kwenye mahabara zikifanyiwa vipimo na majaribio.

    Kwa mujibu wa msomi na mdhadhiri Bwana Omondi Osano, juhudi hizi zitafaulu. Kuhusu mchango na ushirikiano wa China katika kutafuta chanjo na tiba ya virusi vya corona, bwana Omondi anasema kwamba China iko kwenye mstari wa mbele katika juhudi hizi. Hili linadhihirika wazi kutokana na mchango wake kwa Shirika la Afya Duniani (WHO), licha ya kupigwa vita na baadhi ya mataifa.

    Vile vile, China inasema kwamba endapo chanjo itapatikana, basi itashirikiana na ulimwengu wote kuhakikisha kwamba kila taifa linanufaika.

     


    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako