Rais Donald Trump wa Marekani amesaini amri ya kuhimiza idara ya polisi kutumia nguvu kwa kufuata kanuni, wakati maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi jana yakiendelea katika miji mbalimbali nchini humo.
Mapema jana, polisi walitumia vifaa vya kikemikali kuwatawanya waandamanaji 100 mjini St. Cloud, Minnesota na kuwakamata baadhi yao. Maandamano ya kupinga kitendo cha kimabavu cha polisi na ubaguzi wa rangi mjini Portland, Oregon yameendelea kwa siku 20. Maandamano kama hayo pia yanaendelea katika miji ya Atlanta, Tallahassee, Albuquerque na Nashville.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |