Mwendesha mashtaka mkuu wa Russia Igor Krasnov alisema jana mjini Moscow kuwa Russia ilifanikiwa kuvunja majaribio 43 ya shughuli za kigaidi kwenye maeneo 24 ya nchi hiyo mwaka jana, ambayo idadi yake iliongezeka kwa asilimia 38 kuliko mwaka 2018.
Bw. Krasnov amesema hivi sasa Russia inakabiliwa na tishio kubwa la ugaidi, na katika siku zijazo inatakiwa kuimarisha hatua za kupambana na ugaidi kabla ya matukio ya kigaidi kutokea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |