Serikali ya Kenya imelilaumu gazeti la Daily Nation la nchi hiyo kwa kutoa habari zisizo sahihi kuhusu Wachina walioko nchini humo.
Toleo la tarehe 17 la gazeti hilo lilitoa bahari inayosema, Wachina 200 wameondoka nchini Kenya kutokana na kuenea kwa maambukizi ya virusi vya Corona. Ofisa mwandamizi wa habari wa wizara ya mambo ya nje ya Kenya Jane Kariuki amesema habari hizo hazina msingi wowote, hivyo gazeti hilo linapaswa kuomba msamaha.
Ubalozi wa China nchini Kenya na Shirika la Ndege la China Southern pia zimetoa taarifa ya kusema habari hizo sio kweli.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |