Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema, serikali yake itatoa redio bila malipo kusaidia wanafunzi kujisomea majumbani wakati huu wa mlipuko wa maambukizi ya virusi vya Corona nchini humo.
Rais Museveni amesema, wataanzisha mpango wa elimu kwa kupitia vipindi vya radio, na kwamba ingawa alipendelea zaidi kutumia TV, lakini wanasayansi wamesema, TV italeta mkusanyiko wa watu vijijini.
Rais Museveni pia amesema, machapisho ya vitabu vya elimu pia yatatolewa kusaidia wanafunzi kujifunza wakiwa nyumbani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |