Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamelaani vikali shambulizi dhidi ya Tume ya Umoja huo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (MONUSCO), lililotokea Jumatatu karibu na mji wa Beni mkoani Kivu Kaskazini, na kusababisha kifo cha mlinda amani kutoka Indonesia na mwingine kujeruhiwa.
Wajumbe wa Baraza la Usalama wametoa wito kwa mamlaka za DRC kuchunguza mara moja shambulizi hilo na kuwafikisha wahusika mbele ya sheria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |