Waziri wa Utalii na Wanyamapori wa Kenya Najib Balala ametoa wito wa kuwepo na mikakati mipya ya kuvutia watalii wa nje na wa kikanda wakati huu dunia inapokabiliwa na mlipuko wa virusi vya Corona.
Amesema kuendelea kutegemea nchi za magharibi kutakuwa na athari hasi, na badala yake amezitaka nchi za Afrika kufungua mipaka yao na kuwekeza kwenye miundo mbinu ya usafiri ili kusaidia usafiri wa watu barani humo kwa urahisi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |