Wizara ya viwanda, biashara na maendeleo ya makampuni ya Kenya imeahidi kutumia mamlaka ya biashara kulinda viwanda vya ndani kutokana na ushindani wa kigeni usio na usawa.
Waziri wa wizara hiyo Bi. Betty Maina amesema, Mamlaka ya Kurekebisha Biashara ya Kenya (KETRA) itatoa mfumo wa kisheria na kikanuni kulinda viwanda vya ndani kwa mujibu wa sheria ya Shirika la Biashara Duniani WTO.
Bibi Maina pia amesema, Kenya itatekeleza hatua za kulinda biashara kama kupambana na utupaji wa takataka, kulipwa sehemu ya ushuru wa maduhuli na kupambana na uagizaji wa bidhaa unaoharibu viwanda vya ndani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |