Jeshi la Iraq limesema, muungano wa kimataifa unaoongozwa na Marekani umefanya mashambulizi ya anga dhidi ya kambi moja ya kundi la IS mkoani Nineveh, kaskazini mwa Iraq na kuwaua wapiganaji 11. Iraq ilitangaza ushindi wa kihistoria katika mapambano na kundi la IS mwezi Desemba mwaka 2017, lakini hivi karibuni wapiganaji waliobaki wa kundi hilo wamefanya mashmbulizi kadhaa nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |