Waziri mkuu wa Uingereza Boris Johnson ameitaka serikali ya Israel isimamishe mpango wa kukalia sehemu ya kando ya Magharibi ya Mto Jordan, badala yake itatue masuala kwa mazungumzo na Palestina. Kwenye makala yake iliyochapishwa jana katika gazeti la kiyahudi Yediot Aharonot nchini Israel, Bw Johnson amesema hatua hiyo ya Israel ni kinyme cha sheria ya kimataifa, pia inatishia usalama wa Israel yenyewe na juhudi za kimataifa za kuleta amani katika kanda ya Mashariki ya Kati.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |