• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Asilimia 80 ya Warusia wapiga kura za kukubali Vladmir Putin kuendelea kuwa rais hadi mwaka 2036

    (GMT+08:00) 2020-07-02 19:32:32

    Russia jana ilipiga kura ya maoni kwa raia wote juu ya mswada wa marekebisho ya katiba. Matokeo ya takwimu mpya yalionesha kuwa, raia wengi wa Russia walipiga kura za ndiyo za kuunga mkono marekebisho hayo.

    Marekebisho hayo ni pamoja na kuongeza pensheni, kupanga mshahara wa kima cha chini kabisa, na kuondoa kikomo cha muda wa urais. Kama marekebisho hayo yakiidhinishwa, rais wa sasa wa Russia Vladmir Putin mwenye umri wa miaka 67 ataweza kuendelea kuwania uchaguzi wa rais mwaka 2024 na kuendelea kushika madaraka hadi kufikia mwaka 2036.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako