Mkuu wa majeshi ya ulinzi ya Russia Valery Gerasimov na mwenyekiti wa Kamati ya kijeshi ya Jumuiya ya NATO Stuart Peach wamefanya mazungumzo kwa simu, wakijadili hali ilivyo kuhusu usalama wa Ulaya na udhibiti wa silaha. Taarifa iliyotolewa na wizara ya ulinzi ya Russia inasema, masuala mengine yaliyojadiliwa ni pamoja na hatua za kukabiliana na janga la COVID-19 na jinsi ya kuzuia mikwaruzano wakati wa kutekeleza shughuli za kijeshi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |