• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa amteua Cristina Duartc wa Cape Verde kuwa mshauri maalum wa masuala ya Afrika

    (GMT+08:00) 2020-07-03 09:21:31

    Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amemteua Cristina Duartc kutoka Cape Verde kuwa mshauri wake maalum wa masuala ya Afrika.

    Bibi Duartc, anayechukua nafasi ya Bience Gawanas wa Namibia, ana uzoefu wa miaka 34 ya uongozi na usimamizi wa kimkakati katika utungaji wa sera za umma na sekta ya binafsi, pia uelewa mkubwa wa ushirikiano wa kimataifa na wa kikanda, pamoja na changamoto zinazolikabili bara la Afrika.

    Bibi Duarte pia alikuwa waziri wa fedha, mpango na utawala wa umma wa Cape Verde kuanzia mwaka 2006 hadi mwaka 2016.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako